WhatsApp Image 2025-05-21 at 10.01.56
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Kassim amezindua “Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Ufugaji Nyuki kwa Tanzania Iliyobora (Achia Shoka, Tundika Mzinga)”. Kwa lengo la kuongeza viwango vya uzalishaji wa asali kutoka tani 34, 861 hadi kufikia tani 75,000 ifikapo Juni 2035 na kuongeza mauzo ya mazao ya nyuki katika masoko ya kikanda na kimataifa, na kutoa rai kwa wadau wote watakao husika katika mpango hui kuutekeleza kwa weledi, uaminifu na uadilifu mkubwa ili kujenga imani kwa wananchi mmoja mmoja watao amua kuingia katika sekta hii.
WhatsApp Image 2025-05-21 at 10.01.53
WhatsApp Image 2025-05-21 at 10.01.54 (1)
WhatsApp Image 2025-05-20 at 13.50.03
Mhe. Balozi Dk. Pindi Chana Waziri wa Maliasili na Utalii awasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii katika Mwaka wa Fedha 2024/25, katika Kikao cha 27 cha Mkutano wa 19 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
SIFA ZA ASALI YA TANZANIA, ALAMA YA UTAMBULISHO NDANI NA NJE YA NCHI.
SIFA ZA ASALI YA TANZANIA, ALAMA YA UTAMBULISHO NDANI NA NJE YA NCHI.

  Matokeo ya utafiti yaliyofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania TAFORI katika kubaini sifa za asali kwenye uoto mbalimbali hapa nchini yamebaini uwepo wa asali yenye sifa tofauti katika ubora ikiwemo ladha, rangi pamoja na viambata muhimu. Uwepo wa sifa hizi za asali umewezesha kutengenezwa kwa Alama ya Asali ya Tanzania (Honey Trademark) itakayoitambulisha asali hii ndani na nje ya nchi. Haya yameelezwa na Mhe. Balozi Dk. Pindi Chana Waziri wa Maliasili na Utalii wakati akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii katika Mwaka wa Fedha 2024/25, katika Kikao cha 27 [...]

WhatsApp Image 2025-05-20 at 13.48.32 (1)
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule azindua rasmi maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma ,maadhimisho ya siku siku 4 kuanzia Mei 17 hadi 20, 2025
WhatsApp Image 2025-05-20 at 15.28.38 (1)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Dk. Hassan Abbas, Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki Wizara ya Maliasili na Utalii
Bw. Deusdedit Bwoyo, Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI Dk. Revocatus Mushumbusi wakifanya ziara katika mabanda ya taasisi na wajasiriamali wanaotangaza huduma na bidhaa zinazotokana na mazao ya Nyuki kwa ajili ya kubadilishana uzoefu na kupata taarifa kutoka kwa Wataalamu katika siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani Mei 20, 2025 yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, Jijini Dodoma.
WhatsApp Image 2025-05-20 at 13.47.24
Mtaalamu wa Utafiti wa Ufugaji Nyuki kutoka Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) Bw. Stephen Msemo akifanya mawasilisho ya matokeo ya kitafiti kuhusu “Usimamizi wa Makundi ya Nyuki na Manzuki katika Kukuza Uchumi” kwa wadau, wakulima na wafugaji wa Nyuki, kwa ajili ya kuimarisha afya na kujikwamua kiuchumi ikiendana na kauli mbiu ya maadhimisho isemayo “Nyuki kwa Uhai na Uchumi Imara, Tuwahifadhi”. Mei 18, 2025 katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma,
N4
n14
2
ACB
PHOTO-2024-12-04-09-24-50
DAY.1
11112
DAY 3.1
previous arrow
next arrow

Forest and Beekeeping Videos for Stakeholders